20%
❤️ Rita Charity Fund
Fedha zinaelekezwa moja kwa moja kwenye shughuli za kijamii kupitia Rita Charity — kusaidia yatima na
watoto wenye uhitaji. Hukusanywa kila baada ya miezi mitatu kupitia kampeni
“Twendeni, Tuwapelekee Tabasamu” ambapo wadau wanashiriki kuamua kituo cha kutembelewa.
30%
🤝 Ambassador Reward Fund (ARF)
Inawalipa Ambassadors wanaoleta watumiaji wapya kupitia Referral Code. Mfano: Ambassador anapata
30% × Tsh 500 = Tsh 150 kila mwezi kwa kila mtumiaji aliyemleta anayeendelea kulipa
subscription. Malipo hutolewa tarehe 5 ya kila mwezi (kiwango cha chini Tsh 10,000), bila ukomo wa muda.
20%
✍️ Songwriters Support Fund (SSF)
Huwathamini na kuwawezesha watunzi wa nyimbo za Kanisa. Gawio hukokotolewa kwa uwiano wa asilimia ya
downloads za nota (PDF) za kila mtunzi kwa mwezi — mfano, nota yenye 10% ya downloads zote hupata 10% ya
fedha za SSF. Mahesabu hufanyika tarehe 25, malipo tarehe ya mwisho ya mwezi.
20%
📈 Engagement Reward Fund (ERF)
Huzitambua na kuzizawadia kwaya zinazochangia ukuaji wa Muziki Mtakatifu kupitia followers, engagement na
maudhui. Kwaya tatu bora hupokea 30% / 20% / 15%, na kwaya zinazochipukia (emerging) hupokea 20% / 10%,
huku 5% ikiwekwa kama Stabilization & Growth Reserve.